Tuesday, April 16, 2013

JE WAJUA HAPO ZAMANI RUNGU LILITUMIKA KAMA SINDANO YA GANZI?


Kabla wagonjwa waligongwa kwa nguvu kichwani ili wazirai kabla ya kufanyiwa operesheni

HAPO zamani kabla dawa ya kutuliza maumivu wakati wa kumfanyia mgonjwa upasuaji haijavumbuliwa wagonjwa walihisi maumivu makali kwani walifanyiwa huduma hiyo pasipo kuchomwa dawa yoyote; wakilia na kupiga mayowe yaliyojaza chumba kizima cha upasuaji michirizi ya damu iliwarukia madaktari waliotoa huduma hiyo na hata kusambaa chumbani kutokana na kujirusha rusha kwa mgonjwa.
Kulingana na kitabu cha historia kiitwacho "Who did it first" kilichoandikwa na Prof. G. C. Thornley mwenye shahada ya juu ya Phd. katika historia vijana wenye nguvu walihitimiza juu ya meza anapofanyiwa upasuaji.
Cha kushangaza na kuogofya zaidi ni kuwa wagonjwa walioneshwa kuwa waoga na wasumbufu waligongwa na kitu sehemu maalum kichwani ili wazirai halafu daktari akawafanyia upasuaji kwa haraka kabla hawajazinduka pindi walipozinduka kabla ya operesheni haijaisha walijikuta wako kwenye maumivu makali kiasi cha kuwapelekea kulaani ni kwa nini walizaliwa duniani wawe hai kuhisi maumivu hayo.
Profesa Thornley anasema kuwa watu wa kwanza kugundua dawa ya kutuliza maumivu wakati wa upasuaji walikuwa ni Wachina .
Dawa hizi za kienyeji zilizodhaifu na zisingeliweza kumtulizia mgonjwa maumivu inavyotakiwa pia zilikuwa na madhara yake kwani kama ulitumia nyingi kwa makusudi ili mgonjwa asiumie, zilimzidi nguvu na kumuua pia kama ulituma kidogo hazikufaa kitu na mgonjwa alihisi maumvu maradufu.
Baada ya mwaka 1970 Joseph Priestley, kwa mara ya kwanza alivumbua gesi iliyofikiriwa ingelifaa kutumiwa kwa kazi hii. Gesi hiyo ndiyo ile ambayo leo yaitwa "Laughing gas" kwa zaidi ya miaka 30 toka Priestley aivumbue hakuna mtu aliyeitilia maanani.
Lakini mwaka 1800, Sir. Humphry Davy aliweza kuthibitisha faida zake hata akaipa jina ambalo imedumu kuitwa hivyo hata leo "Nitrous Oxide" Sir. Humpherey alipendekeza kuwa gesi hiyo ingefaa kutuliza maumivu wakati wa upasuaji lakini miaka ikazidi kuyoyoma huku kukiwa hakuna daktari aliyechukua hatua za kuitumia kwenye upasuaji.
Lakini kunako mwaka 1824, Daktari mmoja aitwaye Hichman alisoma kwa makini vitabu vya Sir. Humphery ndipo akaamua kuijaribisha gesi hii kwa mbwa na wanyama wengineo.
Akaibuka na matokeo mazuri sana lakini Hichman akafa angali kijana katika umri wa miaka 29 tu.
Baada ya hapo gesi hii iliyojulikana kama "Laughing gas" au "Gesi ya vicheko" ilianza kutumiwa kwenye kumbi za dansi huko Marekani; waliipuliza wakati wa kucheza muziki, ikawalewesha na kuwapelekea kucheka hovyo na kufurahi sana.
Lakini mtu mmoja aitwaye Horace Wells alienda katika ukumbi mmoja wapo wa dansi akawachunguza vijana wale kwa makini na kugundua kuwa walipokuwa wakicheka walikuwa pia hawahisi maumivu hata wakijigonga kwenye vitu.
Horace Wells aliamua kuifanyia gesi hiyo majaribio mwilini mwake. Yeye mwenyewe alijipulizia gesi hiyo ikamlewesha kisha akamwambia rafiki yake amng’oe jino lake moja na huyo rafikie akafanikiwa kumfanyia Horace huduma hiyo pasipo kuhisi maumivu yoyote.
Horace Wells alianza kujivunia ugunduzi wake kote katika Marekani lakini alisahau kitu kimoja kuwa hakuwa na hakika ni kipimo kiasi gani kilihitajika cha gesi ili mtu asisikie maumivu anapong’olewa jino.
Alienda katika shule moja na kauwafanyia wanafunzi majaribio ya kuwang’oa meno kwa kutumia gesi hiyo lakini kila mwanafunzi aliyemfanyia jaribio hilo alilalamika kuwa anahisi maumivu makali .
Well aliamua kurudia jaribio lake kwa mwanafunzi mmoja akidhani kuwa safari ya kwanza labda aliwapa dozi ndogo ya gesi.
Lakini safari hii alijisahau akampulizia gesi kupita kiasi mwanafunzi huyo akafa palepale wakati akimfanyia majaribio.
Tukio hilo lilimchanganya akili Bw. Horace Well aliyependa kusifiwa.
Hivyo Well akapagawa na akachukua hatua ya kujiua mwenyewe kufuatia jaribio lake kushindwa.
Baada ya kifo cha Well daktari mmoja bingwa wa majaribio ya kisayansi aliyeitwa J.Y. Simpson aliona upo umuhimu wa kuiendeleza dawa ya gesi, iliyowashinda wataalam wengi kukamilisha na ni yeye ndiye aliyekuja kufanikiwa kutengeneza dawa ya kwanza ya kupunguza maumivu wakati wa upasuaji.
Simposon alizaliwa katika familia ya wazazi maskini sana lakini mama yake mzazi alitaka kuona mwanaye anakuwa na maisha mazuri siku za usoni.
Walimpeleka katika Chuo Kikuu cha Edinbugh ambako aliweza kusomea shahada zote za juu kabla ya kuamua kujitosa kwenye fani ya Udaktari.
Wakati huo daktari mmoja aitwaye Robert Liston alifanikiwa kumfanyia mgonjwa operesheni ya kukata mguu jijini London kwa kutumia dawa yake iitwayo "Either" Dk Liston alitumia dakika 26 kumkata kabisa mgonjwa huyo mguu naye hakuhisi maumivu hata kidogo.
Simpson alisikia habari za operesheni hiyo hivyo akafunga safari kutoka Edinburgh mpaka London kwenda kuchukua "Either’ aje aifanyie majaribio yeye mwenyewe alifanikiwa kuipata na akarejea nayo jijini Edinburgh ambako yeye na marafiki zake wawili; Duncan na Keih walitumia kwa kuifanyia majaribio gesi hiyo.
Mwanzoni Simpson alitaka kuutumia mwili wake yeye mwenyewe kujaribu gesi hiyo lakini, rafiki zake wakamshauri aijaribishie kwa wanyama kwanza. Hivyo alimjaribishia mbwa naye akazidiwa na kufa.
Baada ya kuifanyia utafiti kwa karibu mwaka mzima Simposon na marafiki zake wawili walijaribisha dawa ya Simposon aliyoiita "Chloroform"na ikamlewesha Simpson mwenyewe kiasi kwamba akajikuta amedondoka uvunguni mwa meza.
Halafu Simposon akarudiwa na fahamu akamuona mwenzake Dk. Duncan akiwa uvunguni mwa kiti akiwa hoi amepoteza fahamu na kuacha mdomo wazi baada ya kuzidiwa na "Chloroform".
Dk. Keith naye pia alikuwa akijikokota baada ya kurudiwa na fahamu.
Hapo ndipo Simpson akajikuta amegundua dawa ya kutuliza maumivu wakati wa upasuaji dawa hii ya "Chloroform"aliyoigundua Simpson ndiyo inayomudu kutumika mahospitalini wakati wa upasuaji hata leo. Haikuwa lelemama hivyo kufikia uvumbuzi huo.