Sunday, April 14, 2013

JOSEPH HAULE

PROF JAY: LAWAMA ZANGU KUHUSU MZIKI UNAPOELEKEA NAZIPELEKA KWA WASANII MASHABIKI MEDIA NA SERIKALI YENYEWE



aah kusema ukweli kitu kikubwa kinachotokea ni kwamba, imefika kipindi sasa imebidi wasanii wa Tanzania inabidi tuamke tuone wapi tunataka tuelekee na pia tuanza kutafakari ni wapi mziki wetu tunataka uelekee, kwasababu tumefanya mziki huu kwa mafanikio, tumetoka mbali kwenye sehem za hatari sana na sasa tuna advantage ya kwamba kiswahili kiswahili kinaenda kama lugha ya kimataifa tumepata mashabiki nje ya tanzania.....".
ndio maana leo kwenye account yangu ya twitter nikasema, inafika kipindi sasa tuangalie, kwasababu kila mmoja anakua anamtupia lawama mwenzake na vitu vingine kama hivi, ni kwamba tukae kama wasanii  kama watanzania tunaotaka tuangalie mziki huu tunataka tuupeleke wapi....
kiukweli inavyoonekana anaeuharibu mziki huu sio mtu mmoja....wasanii kama wasanii unakuta wanaandika mashairi ambayo hayaeleweki hata kwenyejukwaa  perfomance zao vingine havisaidii kuupeleka mziki wetu mbali hata media inaonekana kucheza nyimbo zingine ambazo kiulweli kabisa hazisaiidii chochote kwenye mziki wetu wa Tanzania na  katika harakati hizi za  kuupeleka mziki wetu kwenye level, "
 "lawama zangu pia nazipeleka kwa mashabiki, kwasababu wana nyimbo zao ambazo wanapioga simu wanaomba, kwenye matamasha wanasapoti ya watu wengine lakini kiukweli zile nyimbo hazisaidii chochote, mashabiki saa zingine wanaomba nyimbo ambazo hazisaidii chochote na zinakuwa mbovu, "
"lakini kitu ambacho kikubwa kabisa cha mwisho, ni kwamba serikali ina play part vipi katika swala hili, ikiwa kama baba wa watanzania wote inabidi itoe kauli,kwasababu wasanii kila siku kilio chao ni kwamba kazi zao zinaibiwa watu wanakosa ubunifu ndio maana wanaimba vitu ambavyo viko bubble gum, na vitu ambavyo havieleweki, serikali kama serikali ingejaribu kuangalia jinsi gani ya kuwasaidia wasanii wa Tanzania especially katika kazi zao, kwenye vitu kama ringtones, lakini pia katika sheria jinsi gani msanii anaweza kunufaika na kazi zake anayoifanya, kwasababu hata sasa hivi hizi stika za TRA haziwezi kusaidia kitu stika zitakuwepo lakini tatizo sugu tumeliacha, tatizo ni wizi wa kazi za wasanii......." amesema Prof Jay